Back to top

Wauguzi 4 wa kituo cha afya wasimamishwa kazi kwa kutoa lugha chafu.

06 February 2019
Share

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewasimamisha kazi wauguzi wanne wa kituo cha afya Mkoani wilaya ya Kibaha mkoani Pwani ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili kutoa lugha chafu kwa mama aliyempeleka mwanaye kituoni hapo kupatiwa matibabu na  kuamua kukimbilia hospitali nyingine.

Akizungumzia uamuzi huo mara baada ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya elimu ujenzi na afya kikiwemo kituo cha afya cha Matibwa Bagamoyo Mhandisi Ndikilo amesema  alipokea malalamiko ya mama huyo kufika hospitalini hapo hali ya mtoto ikiwa mbaya lakini wauguzi walishindwa kumsaidia licha ya kuwaomba badala yake kuambulia lugha za kejeli na kuagiza  miundombinu bora ya ujenzi wa vituo kama hivyo uende sambamba na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.