Watendaji wa Wizara ya Afya pamoja na wadau wake wamepigwa marufuku kuwauzia wajawazito vitabu vya kliniki huku Katibu Mkuu wa Wizara hiyo akitakiwa kuhakikisha vitabu hivyo vinapatikana muda wote.....
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Jerry Silaa, ametoa siku thelathini (30) kwa wamiliki wote wa ardhi wanaodaiwa Kodi ya Pango la Ardhi ambao hawajalipa hadi sasa kulipa kodi husika na baada ya muda huo kupita hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmshauri nchini wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo ili kudumisha amani na mshikamano miongoni mwa Watanzania.
Wananchi wanaojishughulisha na uvuvi katika ukanda wa Ziwa Tanganyika, wameunga mkono hatua ya serikali ya upumzishwaji wa shughuli za uvuvi katika ziwa Tanganyika, ili kulipa nafasi ziwa kuongeza kiwango chake cha uzalishaji wa samaki.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Jerry Silaa, amesema Mageuzi makubwa Sekta ya ardhi yanakuja baada ya kushuhudia utiaji saini kati ya Wizara yake na Mtaalamu Mshauri wa Mradi Mkubwa wa Kuimarisha na Kuboresha Miundombinu ya Upimaji na Ramani (LDI) wenye thamani takribani Bil. 150 za Kitanzania.
Mkuu wa Wilaya ya Mlele mkoani Katavi, Alhaji Majid Mwanga, amesema wahusika wote wa ubadhilifu wa fedha za shilingi 39,501, 665 katika Kijiji cha Kibaoni Halmashauri ya Mpimbwe, Wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.