Waziri Mkuu wa Slovakia Robert Fico, ameshambuliwa kwa risasi, akiwa mbele ya jengo la kituo cha kitamaduni ambalo lipo katikati mwa mji wa Handlova....
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ametoa rai kwa wadau wa maendeleo nchini likiwemo Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kuiunga mkono Serikali katika uelekeo wake wa kuwekeza kwenye sekta za uzalishaji ili kuondoa umaskini kwa wananchi.
Shirika la Viwango nchini (TBS), limesema maziwa mbadala ya watoto aina ya Infacare 1, 2 na 3, yamesajiliwa na Shirika hilo, baada ya kuhakiki ubora na usalama wake.......
Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) imekanusha taarifa za ndege yake aina ya Boeing 787-8, yenye usajili namba 5H-TCJ, kupelekwa kwenye matengenezo makubwa (Check - C), kabla ya kufikisha muda wake tangu inunuliwe na kutelekezwa nchini Malaysia.......
Waziri wa Viwanda na Biashara,Mhe Dkt. Ashatu Kijaji, amesema Serikali inaendelea na mchakato wa kuandaa mfumo mmoja wa ukusanyaji wa kodi kwa wafanyabiashara nchini, ili kuondoa kero ya taasisi mbalimbali za Serikali kukusanya kodi.
Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) wamewakumbusha wananchi, wasafiri, wasafirishaji na watumiaji wengine wa barabara kusafiri kwa tahadhari, haswa wakati huu wa mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali.