Mkapa anaagwa kihistoria uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Rais Magufuli tayari anawaongoza viongozi wa ndani na nje ya nchi katika misa na kuaga mwili wa marehemu Benjamini William Mkapa katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Mwili wa Marehemu Mkapa utasafirishwa leo kupelekwa Kijijini kwao Lupaso na kesho Julai 29 ndio atapumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.