Abiria wakanyaga maji wakiingia ndani ya kivuko Geita.

Abiria wanaotumia kivuko cha MV. Chato Na.1 kinachotoa huduma ya usafiri kutoka Chato kwenda Senga na hatimaye Nkome katika mkoa wa Geita wakiingia ndani ya kivuko hicho kwa kukanyaga majini baada ya gati la Nkome kumezwa na maji kufuatia ongezeko la kina cha maji ya Ziwa Victoria. 
.
Serikali kupitia Wakala wa Umeme na Ufundi TEMESA, wameombwa kuharakisha ujenzi wa gati hilo.