JKT kudhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji.

Kamati ya Ulinzi na Usalama ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi. Siriel Mchembe imekiagiza Kikosi cha Jeshi 835 cha JKT Mgambo kilichopo Kabuku kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kudhibiti migogoro baina ya wakulima na wafugaji iliyokithiri wilayani humo ambayo imesababisha mauaji ya mkulima hivi karibuni.