Waliokwapua fedha za wakulima wa Korosho Ruvuma waanza kuzirejesha.

Viongozi wa vyama vya msingi katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma ambao wanatuhumiwa kuiba fedha za wakulima wa Korosho msimu uliopita, wameanza kurejesha fedha hizo wakiwemo viongozi wa vyama Mruji na Namsosa ambao fedha za wakulima zaidi ya milioni tatu zilipotelea mikononi mwao.