Dkt. Shoo: watanzania endeleeni kupanda miti.

Askofu Mkuu wa KKKT Dkt. Fredrick Shoo amewataka watanzania kuendelea kupanda miti na kutunza mazingira ili kurudisha uoto wa asili ambao umepotea na kusababisha mabadiliko ya tabianchi na ukame katika maeneo mbalimbali nchini hali ambayo ameitaja kuwa ndio chanzo cha machafuko ya hali ya hewa na kukosekana kwa mvua za uhakika.