Gesi yaua wanne Mwembe Togwa mkoani Kigoma.

Watu wanne wamefariki baada ya mtungi wa gesi kulipuka wakati mafundi gereji eneo la Mwembe Togwa mkoani Kigoma walipokuwa wakijaza katika mtungi wa kuchomelea.

Kamanda wa polisi mkoani humo Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akitoa tahadhari kwa wafanyabiashara wa kubadilisha mitungi hiyo kufanyabiashara katika maeneo yaliyombali na makazi ya watu.

Endelea kufuatilia taarifa zetu kufahamu zaidi.