Majambazi wabeba tairi za gari la Kamanda wa polisi Geita.

Jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia majambazi wawili huku likiendelea kuwasaka watu kadhaa kwa tuhuma za kuvamia usiku wa manane eneo lililokuwa limehifadhiwa gari la kamanda wa polisi mkoa huo na kuiba matairi yake yote manne kisha kutokomea pasipojulikana.


Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Mponjoli Lotson anasema katika hali isiyo ya kawaida watu hao kwa kushirikiana na walinzi walifanya uporaji huo  kwa kufungua matairi hayo kisha kutokomea nayo huku jeshi hilo likiendelea na msako ili wahusika wote wakamatwe na kuchukuliwa hatua.