Waziri mkuu amwakilisha Rais jukwaa la vijana.

Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa amemwakilisha Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa njia ya mtandao kwenye Mkutano wa Jukwaa la Nne la Vijana Duniani lililoanza leo jijini Sharm-El-Sheikh, Misri ambapo ameyaomba mataifa makubwa duniani yashirikiane na nchi za Afrika ikiwemo Tanzania ili kuhakikisha uchumi wa nchi hizo unarejea katika hali yake ya kawaida kutokana na madhara ya UVIKO-19.