Back to top

News

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya mwenendo wa kimbunga "HIDAYA" kilichopo karibu na maeneo ya Pwani ya nchi ambapo hadi kufikia saa 9 usiku wa kuamkia leo, Kimbunga "HIDAYA" kilikuwa katika eneo la bahari takribani kilomita 125 kutoka Pwani ya Kilwa (Mkoa wa Lindi), kilomita 93 kutoka pwani ya Mafia na kilomita 128 kutoka pwani ya Dar es Salaam kikiwa na mgandamizo wa hewa wa kiasi cha 985 hPa na kasi ya upepo unaofika kilomita 120 kwa saa.