Back to top

News

#HABARI: Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imezindua rasmi programu ya kitaifa ya utoaji wa chanjo na utambuzi wa mifugo kwa Mkoa wa Songwe, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo kwa Mifugo iliyoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ziara yake mkoani Simiyu. Kupitia programu hiyo, zaidi ya ng’ombe 479,800 na kuku zaidi ya milioni 2.3 wanatarajiwa kunufaika katika Mkoa wa Songwe pekee, ikiwa ni sehemu ya mpango unaotekelezwa nchi nzima.