Back to top

Mama ajifungulia vichakani baada ya mto kujaa Rukwa.

24 March 2020
Share

Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Rukwa zimeendelea kusababisha adha kwa wananchi baada ya kusababisha vifo  vya watu  wawili  na nyumba saba kubomoka katika wilaya ya Kalambo na huku ikisababisha kukatika kwa  mawasiliano ya  barabara ya Kasisiwe katika manispaa ya Sumbawanga na kupelekea mama mjamzito  kujifungulia  vichakani baada ya mto kujaa maji.

Meneja wa wakala wa barabara za vijijini  na mijini (TARURA) mkoani Rukwa Eng. Seth Mwakyembe , amesema, serikali imejipanga  kufanya marekebisho ya madaraja yote ikiwemo daraja la kasisiwe huku mkuu  wa  wilaya ya kalambo julieth binyura akiwataka wananchi kutovuka  kwenye mito iliyojaa maji.