
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), limetoa taarifa kwa wateja wake kuwa kutakuwa na Upungufu wa uzalishaji wa umeme kwa takribani 345MW, ambayo ni sawa na 21% ya uzalishaji wote. Hali hiyo inatokana na mabadiliko ya hali ya hewa ambapo viwango vya maji katika mito na mabwawa yanayotumika kuzalishia umeme ikiwemo vituo vya Kihansi, Kidatu na Pangani vimepungua.

