Back to top

Tanzania, Kenya kumaliza vikwazo vya kiutawala .

18 October 2021
Share

Tanzania na Kenya zimedhamiria kumalizia kuondoa vikwazo vya kiutawala vilivyosalia ifikapo Disemba 2021 baada ya kuondoa vikwazo 46 visivyokuwa vya kikodi.

Hayo yamesemwa wakati wa mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Mhe. Dany Kazungu jijini Dar es Salaam ambapo takwimu zinaonesha urari wa biashara kati ya Nchi hizo umeongezeka mara sita zaidi baada ya kuondolewa kwa vikwazo hivyo.

Kutokana na hatua hiyo, Tanzania imeonekana kunufaika zaidi kwa kuondolewa kwa vikwazo hivyo kwa kuuza zaidi bidhaa zake nchini Kenya.