Back to top

Waganga wa jadi waitwa Tunduru kufukuza Tembo mashambani

07 November 2019
Share

Wananchi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wanaendelea kusumbuliwa na Tembo wanaoharibu mazao yao na kusababisha vifo  ambapo kutokana na changamoto hizo baadhi yao wameanza kuwaita waganga wa jadi kusaidia  kuzuia na kuwafukuza tembo mashambani kwa njia za kishirikina.

Kutokana na changamoto hizo shirika la uhifadhi wa maliasili na mazingira la  Pams Foundation limetoa semina elekezi kwa wananchi juu ya teknolojia ya kufukuza Tembo kwa kutumia pilipili,oil chafu na kuchoma tofali la pili pili
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Tunduru Bw. Julius Mtatiro amewataka wananchi kuacha kuamini kwamba Tembo anaweza kuzuiwa  kwa kutumia ushirikina