Back to top

Watu wanne wamefariki Namasalau Tunduru kwa ugonjwa wa ajabu

23 October 2018
Share

Watu wanne katika kijiji cha Namasalau kata ya Tuwemacho wilayani Tunduru  mkoani Ruvuma  wamefariki dunia kwa kuugua  ugonjwa wa ajabu wa kukohoa na kutapika damu huku wananchi  wakiuhusisha ugonjwa huo na ushrikina.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Bw. Juma Homera ametembelea kijiji hicho kujionea hali halisi na amesema serikali imechunguza ugonjwa huo na bado haujabainika ni ugonjwa gani na kwamba uchunguzi bado unaendelea huku wananchi  wakitaka awaletee awaletee mganga wa  kienyeji.