Back to top

WAWILI WAFARIKI KWA AJALI YA NDEGE, SELOUS

18 May 2023
Share

Watu wawili wamefariki huku wengine wawili wakijeruhiwa kufuatia ajali ya ndege ya Shirika la Frankfurt Zoological aina ya Cessna 182 yenya namba za usajili 5H-FZS, iliyoanguka muda mfupi baada ya kuruka kwenye kiwanja kidogo cha ndege cha Matambwe, Selous.
.
Timu ya uchunguzi wa ajali kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini (TCAA) imeshaanza uchunguzi kujua chanzo cha ajali hiyo na itatoa taarifa kwa mujibu wa sheria.