
Jaji Joachim Tiganga anayesikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi na Vitendo vya Kigaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe.Freeman Mbowe ameahirisha kesi hiyo mpaka Jumatatu Novemba 22 kwa ajili ya kupata muda kupitia pingamizi kuhusiana na kielelezo cha upande wa mashtaka ambacho ni kitabu cha kumbukumbu cha Mahabusu ambacho mawakili wa utetezi walipinga kisipokelewe na Mahakama kwa Madai kilikiuka utaratibu wa sheria.
