Mwili wa Mfanyabiashara wa vitunguu Jackson Charles aliyeripotiwa kupotea tangu Oktoba 22 mwaka huu huko wilayani Wangingombe mkoani Njombe umekutwa katika msitu wa Ngaramaro kijiji cha Mtapa wilayani humo na kusafirishwa kwenda kuzikwa kwao wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Kwa mujibu wa uongozi wa Kata ya Kidugala wilayani Wangingombe ambako marehemu alikuwa anafanyia biashara mwili wa mfanyabiashara ulikutwa katika msitu huo ukiwa umeharibika na baaadhi ya viungo vikiwa havipo na serikali ikachukua jukumu la kuuzika hapo Desemba 5 mwaka huu.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issa amethibitisha kushikiliwa kwa mtuhumiwa mmoja kutokana na tukio hilo.
