
Ghala la kuhifadhia magodoro linalomilikiwa na Kampuni ya Vitanda Manufacturing Tanzania Ltd ya Jijini Mwanza, lililopo Mtaa wa Milanzi Mjini Tabora limeteketea kwa moto ambao haujajulikana chanzo chake, ambapo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Richard Abwao amebainisha kuwa tukio hilo halijasababisha madhara kwa binadamu.
