Klabu ya Everton imethibitisha kuwa mchezaji wao Andre Gomes baada ya kuumizwa vibaya Jana akiwa uwanjani dhidi ya Tottenham amefanyiwa upasuaji na umekamilika vizuri.
Mchezaji huyo alichezewa rafu na Son wa Tottenham Hotspurs iliyomtegua kifundo cha mguu wake katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 ndani ya dimba la Goodson Park.
Klabu ya Everton imethibitisha kuwa Andre Gomes upasuaji wake umekamilika salama.
Atakuwa nje ya uwanja kwa ajili ya kupata matibabu zaidi hospitalini.
Aidha klabu ya Everton imewashukuru mashabiki waliokuguswa na tukio hilo hasa kwa arafa za pole kwenye mitandao ya kijamii.