Mamia ya abiria wa treni ya reli ya kati kutoka Kigoma kuelekea mikoa ya bara wamekwama mjini Dodoma kwa zaidi ya saa kumi baada ya reli hiyo kuzibwa na mabehewa ya mizigo yaliyodondoka eneo la Igandu Dodoma.
ITV imefika katika stesheni ya Dodoma na kuzungumza na abiria hao ambao wamesema wanakutana na changamoto ya huduma duni ya chakula na vyoo katika eneo hilo.