Back to top

Askari JWTZ aua askari mwenzake na raia kwa risasi

28 December 2018
Share

Watu wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Ruvuma  yakiwekiwemo ya askari magereza  wa gereza la Kitai wilayani Mbinga mkoani Ruvuma  aitwaye Adam Kunwa kujiua kwa kujipiga risasi kichwani akiwa lindoni kwenye gereza la Kitai  na askari wa jeshi la wananchi wa tanzania  kumuua  mwanajeshi mwenzake pamoja na  raia kwa kuwapiga risasi.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma SACP Gemini Mushy amesema kuwa  mnamo disemba  27 majira ya jioni katika kambi ya jeshi la wananchi wa tanzania ya Chandarua wilayani Songea askari wa JWTZ Juma Mkele akiwa kazini pamoja na  raia Veronika Kayombo waliuawa kwa kupigwa risasi na askari mwingine wa JWTZ aitwaye Batisin Samda akitumia bunduki aina ya SMG.

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kusubiri uchunguzi wa daktari na kwamba upelelezi wa polisi unaendelea kuhusiana tukio hilo.

Katika tukio jingine kamanda Mushy amesema  askari magereza aitwaye Adam Kunwa ambaye ni mganga katika zahanati ya  ya gereza la Kitai akiwa  lindoni  alijiua kwa kujipiga risasi kichwani na kufariki na  upelelezi wa polisi unaendelea.

Tukio jingine kamanda Mushy anabainisha kuwa mkazi wa kijiji cha Namahoka wilayani Namtumbo Bi. Zainabu Mohamed aligongwa na pikipiki  wakati anavuka barabara na kupoteza maisha  huku dereva wa piki piki iliyosabaisha ajali  ambaye jina lake alikufahamika  akitelekeza piki piki na kukimbia.

Wakati huo huo kamanda Mushy  amesema jeshi la polisi limewafukuza kazi askari polisi wake  watatu waliokuwa wakifanyia kazi wilayani Tunduru  kwa makosa ya utovu wa nidhamu kinyume na mwenendo mwema wa jeshi la hilo ambao ni  Robert Elias Mkindo,Alex Sukuma Tenga na  na Charles Anderson Magereja.