Back to top

Babu ajeruhiwa akijaribu kuokoa uhai wa mjukuu bila mafanikio Ruvuma.

10 September 2019
Share

Mtoto Fitina Tukolyese mkazi wa Tunduru mkoani Ruvuma amefariki kwa kuungua moto huku babu yake  aitwaye Greyson Mtendele akijeruhiwa na kulazwa katika kituo cha afya Nakapanya baada ya kujitosa kwenye moto kumuokoa mjukuu wake bila mafanikio huku nyumba saba zikiteketea kwa moto   na kuwaacha wakazi 33 kukosa mahala pa kuishi.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Simon Maigwa Marwa amesema mtoto Fitina Fadhil Tukolyese mwenye miaka miwili na miezi mitano amefariki kwa kuungua moto katika kijiji cha Mkowela  alikomtembelea babu yake mzee Mtendele ambaye amejeruhiwa kwa moto wakati akijaribu kumuokoa mjukuu wake huyo.

 

Wakazi wa Tunduru mkoani Ruvuma wakiwa nje ya nyumba zao baada ya kuungua moto uliotokana na watu kuandaa mashamba na kusababisha nyumba hizo kuungua baada ya upepo kuwa mkali na moto kukamata kwenye nyumba za nyasi, huku mtoto mmoja wa miaka 2 akifariki.