
Waziri wa Ujenzi Mh.Innocent Bashungwa, ametoa saa tatu kwa Wakala wa Barabara (TANROADS) kuhakikisha wanarejesha mawasiliano ya barabara ya Mtwara-Mingoyo-Masasi, ambayo yamekatika baada ya daraja lililopo eneo la Maili Mbili, kusombwa na maji, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
.
Bashungwa ametoa agizo hilo wilayani Masasi, akiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mh.Deo Ndejembi, walipofika katika eneo hilo ambalo watumiaji wa barabara walikwama tangu Asubuhi.
.
“Natoa saa tatu kwa TANROADS kuhakikisha inakamilisha kujenga barabara ya mbadala ili magari na wananchi waanze kupita", Waziri Bashungwa.
.
Naye, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Deo Ndejembi amesema kiasi cha Shilingi Bilioni 30 zimetolewa na Rais kwa ajili ya dharura za matengenezo ya barabara nchi nzima kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA).
