Back to top

Bodi ya Tanesco yaridhishwa na upatikanaji umeme - Mtwara.

06 May 2021
Share

Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO)  imeridhishwa na uimarikaji wa   umeme katika mkoa wa Mtwara  uliyotokana  ongezeko la matumizi  kutoka Mega Watt 12.5 mwaka 2017 hadi Mega Watt 14  mwaka  2021.

Kauli  hiyo ya kuridhishwa  ya upatikana ji wa umeme imetolewa na mwenyekiti wa bodi hiyo ya TANESCO  Dk. Alexandar  Kyaruzi  ambao wako Mtwara kutembelea miradi ya umeme na ufanyaji kazi wake.

Amesema  uimarikaji wa umeme katika mkoa wa Mtwara unakwenda sambamba na idadi kubwa ya mikoa mingine hapa nchini na kusisitiza kuwa lengo la shirika hilo ni kuona vijiji vyote nchini vinaunganishiwa umeme.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Masasi na Nanyumbu mkoani Mtwara wamesifu serikali kwa juhudi zilizochukuliwa na kufanikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika ambao utachochea wawekezaji mbalimbali katika maeneo hayo.