Back to top

Bunge la Marekani limepiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Trump.

14 January 2021
Share

Bunge la uwakilishi nchini Marekani limepiga kura ya kutokuwa na imani dhidi ya rais Donald Trump kwa kuchochea ghasia zilizosababisha uvamizi wa jumba la bunge la Capitol.

Wabunge 10 wa chama cha Republican walishirikiana na wenzao wa chama cha Democrat kupitisha kura hiyo ya kumshtaki rais kwa 232 dhidi ya wabunge 197 waliopinga hatua hiyo.

Ni rais wa kwanza katika historia ya Marekani kupigiwa kura ya kutokuwa na imani mara mbili ama kushtakiwa kwa makosa ya uhalifu na bunge hilo la Congress.

Rais Trump ambaye ni mwanachama wa Republican sasa atakabiliwa na kesi katika bunge la seneti ambapo iwapo atapatikana na hatia huenda akapigwa marufuku kushikilia wadhfa wowote wa ofisi ya umma.

#BBC Swahili