Back to top

Bunge laagiza sheria zote zenye dosari zifanyiwe marekebisho.

13 September 2018
Share

Bunge limeagiza kuwa wizara zote ambazo sheria zake zimeonekana kuwa na dosari katika utelezaji wake kupitia majedwali  yaliyopitishwa na bunge hilo zifanyiwe marekebisho ili kuondoa dosari hizo ili malengo yaliyokuwa yamekusudiwa yaweze  kutimia.

Akiwasilisha taarifa ya kamati ndogo kuhusu uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa katika mkutano wa kumi na moja wa  bunge Mwenyekiti wa kamati hiyo Mh.Andrew Chenge amesema marekebisho hayo yatasaidia sheria hizo kutumiwa vyema.

Awali kabla ya bunge kufanya mazimio hayo baadhi ya wabunge walipata wasaa wa kuchambua marekebisho hayo.

Aidha katika kikao hicho Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage alitoa Bungeni taarifa ya sukari  kuhusu upatikanaji wake na sababau za bei ya sukari kupanda.

Kufuatia taarifa hiyo baadhi ya wabunge walitoa maoni yao na kusema kuna haja ya serikali kuona ni hatua gani za kufanya  ili kuhakisha bei ya sukari inashuka sambamba na kuhakisha upatikanaji wake unakuwa wa uhakika.