Back to top

BURKINA FASO NA URUSI KUSHIRIKIANA KIJESHI

01 September 2023
Share

Rais wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Urusi Yunus-bek Yevkurov.
.
Mazungumzo hayo yamedaiwa kulenga zaidi masuala ya usaidizi wa kijeshi ikiwa ni pamoja na mafunzo kwa maafisa na marubani wa Jeshi la Burkina Faso.
.
Ziara hiyo iliyoongozwa na Waziri Yunus-bek, ni moja wa ufuatiliaji wa mazungumzo yaliyofanyika kati ya Rais Traoré na Rais Vladimir Putin katika mkutano wa Viongozi wa Afrika na Urusi uliofanyika St Petersburg, nchini Urusi.