Back to top

Corona yaendelea kugharimu maisha ya watu, vifo vyafikia 1,384

14 February 2020
Share

China imetoa taarifa mpya kuhusiana na ugonjwa wa Virusi vya Corona ambapo vifo zaidi ya 121 vimeripotiwa kati ya hivyo vifo 116 vikitokea katika mjiwa Hubei pekee.

Tume ya afya nchini humo imesema kuwa mpaka sasa vifo vilivyotokana na ugonjwa huo nchini humo vimefikia 1,384

Leo Ijumaa kuna taarifa mpya 64,456 za maambukizi mapya ya ugonjwa huo wa virusi vya Corona, huku wanaoendelea kuimarika afya zao wakifikia 7,101

Nayo nchi ya Vietnam imeamuru kufungwa  mji mkuu Hanoi, na kuwa eneo la kwanza nje ya Uchina kuwekwa chini ya karantini kwa siku 20.