Back to top

DC Maswa Atakiwa kuchunguza gharama za kujenga jengo la miradi.

12 January 2021
Share

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mh Mwanaidi Ali Khamis amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Maswa  mkoani Simiyu, Bw.Aswege Kaminyoge achunguze gharama zilizotumika kujenga jengo la utawala la miradi ya kimkakati ya Chaki na Vifungashio wilayani humo, baada ya kutoridhishwa na  gharama zilizotumika ikilinganishwa na jengo hilo lilivyo.
.
Aametoa agizo hilo mjini Maswa, baada ya kukagua ujenzi wa  miundombinu ya miradi hiyo inayofadhiliwa na Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa  gharama ya zaidi ya shilingi bilioni nane.
.
Amesema jengo hilo lililokamilika kwa asilimia 93 ni la kawaida sana na haliwezi kugharimu  shilingi milioni mia moja sabini na nane fedha ambazo amesema ni nyingi ikilinganishwa na thamani ya jengo hilo  ambalo mpaka sasa limejengwa kwa gharama ya shilingi milioni mia moja na kumi kwa kutumia mfumo wa Force  Account.
.
Aidha, amemuagiza Mkandarasi wa SUMA JKT anayesimamia ujenzi wa Kiwanda cha Chaki na vifungashio  ahakikishe ujenzi wa majengo ya mradi huo yanakamilika ifikapo tarehe 15 mwezi  Januari, 2021 kama alivyoelekeza Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  Mheshimiwa Selemani Jafo, ili kazi ya kufunga mitambo ya  kiwanda hicho ifanyike na  kuanza uzalishaji.