Back to top

DK.MPANGO:KUDHIBITI RUSHWA UNAHITAJIKA UONGOZI IMARA

18 January 2024
Share

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema katika kudhibiti rushwa unahitajika uongozi imara pamoja na kuishirikisha jamii na wadau kuanzia ngazi ya watoto shuleni.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akishiriki mjadala wa ngazi ya juu uliyohusu masuala ya Utawala Bora na kukabiliana na Rushwa uliyofanyika katika Mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) unaofanyika Davos nchini Uswisi. 

Amesema rushwa imekua changamoto kubwa inayoleta madhara zikiwemo rushwa za ndani ya mataifa na zile za kimataifa.

Akitoa uzoefu wa Tanzania katika kupambana na rushwa, Makamu wa Rais amesema serikali imeweza kuendelea kufanikiwa kupunguza kiwango cha rushwa kwa kuimarisha taasisi za utawala kama vile ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa kuhakikisha anawezeshwa kwa rasilimali fedha na rasilimaji watu, vifaa na uwezo wa kutumia teknolojia ili aweze kufutilia matumizi ya serikali.