Back to top

FBI YAWAFUKUZA KAZI MAAFISA10 WALIOSHIRIKI KUMCHUNGUZA TRUMP

27 February 2026
Share

FBI imewafukuza kazi takriban maafisa 10, ambao wote walishiriki katika uchunguzi kuhusu jinsi Donald Trump alivyoshughulikia nyaraka za siri baada ya muhula wake wa kwanza.

 

Kusitishwa kwao kazi Jumatano, kumethibitishwa na CBS, na kulitangazwa muda mfupi baada ya mkurugenzi wa FBI, Kash Patel, kuiambia Reuters kwamba maafisa hao wa shirikisho walimchunguza alipokuwa raia wakati wa uchunguzi wa hati hizo.

 

Patel hakutoa ushahidi wowote wa makosa yaliyofanywa na wafanyakazi wa FBI waliofukuzwa kazi.

 

Baada ya Trump kuondoka Ikulu ya White House mwaka 2021, Wakili Maalum Jack Smith aliongoza uchunguzi dhidi ya Trump ambaye sasa ni Rais. Kesi moja ililenga kujua ikiwa Trump alijaribu kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa 2020.

 

Nyingine ilihusisha hati za siri ambazo Trump alizipeleka katika makazi yake ya Mar-a-Lago huko Florida na juhudi zake za kuzuia Wizara ya Sheria ya Marekani kuzipata.

 

Wafanyakazi wa FBI waliofutwa kazi Jumatano wote walishiriki katika kesi juu ya hati za siri.

 

Trump na washirika wake wawili walishtakiwa mwaka 2023, kufuatia uchunguzi wa Smith kuhusu hati hizo.

FBI imewafukuza kazi takriban maafisa 10, ambao wote walishiriki katika uchunguzi kuhusu jinsi Donald Trump alivyoshughulikia nyaraka za siri baada ya muhula wake wa kwanza.

 

Kusitishwa kwao kazi Jumatano, kumethibitishwa na CBS, na kulitangazwa muda mfupi baada ya mkurugenzi wa FBI, Kash Patel, kuiambia Reuters kwamba maafisa hao wa shirikisho walimchunguza alipokuwa raia wakati wa uchunguzi wa hati hizo.

 

Patel hakutoa ushahidi wowote wa makosa yaliyofanywa na wafanyakazi wa FBI waliofukuzwa kazi.

 

Baada ya Trump kuondoka Ikulu ya White House mwaka 2021, Wakili Maalum Jack Smith aliongoza uchunguzi dhidi ya Trump ambaye sasa ni Rais. Kesi moja ililenga kujua ikiwa Trump alijaribu kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa 2020.

 

Nyingine ilihusisha hati za siri ambazo Trump alizipeleka katika makazi yake ya Mar-a-Lago huko Florida na juhudi zake za kuzuia Wizara ya Sheria ya Marekani kuzipata.

 

Wafanyakazi wa FBI waliofutwa kazi Jumatano wote walishiriki katika kesi juu ya hati za siri.

 

Trump na washirika wake wawili walishtakiwa mwaka 2023, kufuatia uchunguzi wa Smith kuhusu hati hizo.

 

2024, jaji wa shirikisho huko Florida alifuta kesi dhidi ya Trump, baada ya kugundua kuwa Smith aliteuliwa kinyume cha sheria.

 

Mwaka huu, mahakama ya rufaa ya shirikisho huko Georgia ilifuta kesi dhidi ya washtakiwa wawili wa mwisho kwa ombi la wizara ya sheria ya Trump.

 

Tangu Trump aliporejea Ikulu ya White House mwezi Januari, wizara ya sheria na FBI wamewafukuza kazi wafanyakazi walioshiriki katika uchunguzi dhidi yake.

 

Wizara ya sheria pia imefungua mashtaka dhidi ya mkurugenzi wa zamani wa FBI James Comey, ambaye Trump alimfukuza kazi wakati wa muhula wake wa kwanza mwaka 2017, na Mwanasheria Mkuu wa New York Letitia James, ambaye aliongoza kesi dhidi ya Trump.