
Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, linawashikilia watu watatu, kwa tuhuma za kumteka mtoto mwenye umri wa miaka minne, kisha kumficha, wakishinikiza kupewa Tsh. Mil. 4 ,ili waweze kumuachia.
.
Akitoa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Bi.Safia Jongo , amesema tukio limetokea huko wilayani Mbogwe, na kwamba watekaji hao walitoa siku nne wawe wametumiwa fedha hizo, lakini Jeshi hilo limepambana na kufanikiwa kuwakamata ndani siku tatu.
