
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amewaomba Southampton waifunge Liverpool mabao 4-0 katika mchezo wao utakaochezwa siku ya Jumanne kwenye Ligi Kuu ya Uingereza.
.
Maombi hayo ya Guardiola yanafuata baada ya Manchester City kutoka sare ya bao 2-2 na West Ham United huku kocha huyo akiulizwa kama ana ujumbe wowote kwa Liverpool.
