Back to top

Hospitali za misheni Songea zatakiwa kutoa huduma kwa gharama nafuu.

17 May 2018
Share

Mkuu wa wilaya ya Songea Bw. Pololeti Mgema amewataka wasimamizi wa hospitali,zahanati na vituo vya afya  zinazomilikiwa  na na madhehebu ya dini wilayani humo  kuhakikikisha wanatoa huduma kwa gharama nafuu kulingana na msamaha wa kodi wanaoupata  wanapoagiza vifaa na madawa kutoka nje ya nchi.

Bw. Mgema ameyasema hayo wakati akizindua mashine ya kisasa ya kuchomea taka ya hospitali ya Rufaa ya misheni peramiho iliyonunuliwa toka Korea  Kusini kwa zaidi ya shilingi Milioni  200  ambapo katika wilaya ya Songea Kanisa Katoliki linamiliki vituo vya afya,zahanati na hospitali nyingi  mijini na vijijini likisaidiana na serikali katika kutoa huduma za afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa hospitali ya  Rufaa ya misheni Peramiho Dk Ansigar Stuffe amesema wamenunuma mashine hiyo ili kutunza mazingira na kuondoa athari  za taka kwa wagonjwa na wanakuja kuuguza wagonjwa kwa kuwa mashine hiyo haitoi moshi wakati wa kuchoma taka.