Back to top

Kikosi cha doria ya uvuvi chakamata kilo 951 za samaki wadogo.

26 January 2021
Share

Kikosi cha doria cha ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi kanda ya Simiyu na Magu  kimekamata kilo 951 za  samaki wadogo aina ya sangara wenye thamani ya shilingi milion tatu ambao wamevuliwa kinyume cha sheria ya uvuvi namba 22,2003.
.
Kufuatia kukamatwa kwa samaki hao Afisa Usimamizi wa doria kanda ya Simiyu na Magu Hamad Stima ametoa wito kwa wavuvi na wafanyabiashara ya samaki  kufuata sheria za uvuvi na kuacha kujihusisha na uvuvi haramu.