
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw.Tundu Lissu amesema anatarajia kurejea Tanzania, Januari 25, 2023 akitokea nchini Ubelgiji.
.
Lissu ameyasema hayo, wakati akitoa salamu za mwaka mpya 2023, kupitia mtandao wa Zoom, ambapo amebainisha kuwa atakanyaga udongo wa ardhi ya Tanzania kwa mara nyingine, siku ya Jumatano, Januari 25, 2023, saa 7:35 mchana.
