
Lori aina ya Howo, Tiper lenye namba za usajili T 459 EBX, mali ya kampuni ya CRCG inayojishughulisha na uchimbaji wa makaa ya mawe, lenye thamani ya Tsh. Mil. 150/=, lililoibiwa mkoani Ruvuma, limepatikana katika Kata ya Ramadhan iliyopo mkoani Njombe.
.
Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma ACP Marco Chilya, amesema tayari wamemkamata Dereva wa lori hilo, ambaye pia alihusika na wizi huo, na kwamba upelelezi umekamilika na atafikishwa mahakamani kesho Juni 16, 2023.
