Back to top

LUKUVI ATEULIWA KUWA MSHAURI WA RAIS

13 June 2023
Share

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa washauri wa Rais (Siasa na Uhusiano wa Jamii) wanne, akiwemo Mhe.William Lukuvi - Mbunge wa Jimbo la Ismani, Bw.Abdallah Bulembo - Mbunge Mstaafu, Balozi Rajab Omar Luhwavi - alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji na Bw.Haji Omar Kheir - Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.