Back to top

Madereva Bodaboda watakiwa kufuata sheria ili kuepuka ajali

10 August 2018
Share

Kamanda wa polisi wa wilaya ya Mbinga  SSP Ramia Mganga  amewataka madereva bodaboda wilayani humo  kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuzuilika kwa kufuata sheria.
  
Pamoja na wito  huo kwa waendesha bodaboda  SSP Ramia Mganga pia amewataka  maofisa elimu Kata waliokabidhiwa pikipiki na serikali  hivi karibuni  kufuata sheria na kutozitumia pikipiki hizo kufanyia biashara na kwamba watapokiuka sheria hatua  zitachukuliwa dhidi yao.
 
Wakati huo huo  mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF nao unawaasa waendesha boda boda kujiunga nao ili kutibiwa kwa gharama nafuu pindi wanapopata ajali.