Back to top

MAHAKIMU, MAJAJI WAPOKEA RUSHWA KWA MIAMALA YA SIMU

22 January 2023
Share

Baadhi ya Mahakimu na Majaji katika ngazi mbalimbali za mahakama mkoani Mbeya, wamedaiwa kubuni njia mpya za kupokea rushwa, ikiwemo ya kutumia miamala ya simu zisizokuwa zao , ili kuficha utambulisho wao, pale wanapofuatiliwa na vyombo vya dola.
.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dkt.Rashid Chuachua, wakati akifungua maadhimisho ya Wiki ya Sheria katika mahakama kuu kanda ya Mbeya.