
Abiria zaidi ya 60, walioukuwa wakisafiri kutoka wilayani Lushoto, kwenda mkoani Dar es Salaam kwa kutumia basi la kampuni ya Maning Nice, lenye namba za usajili T 122 DEA, wamenusurika kifo baada ya breki za basi hilo, kushindwa kufanya kazi kwenye mteremko mkali wa milima ya Usambara, mkoani Tanga.
.
ITV imezungumza na dereva wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Twariki Abdallah, ambaye amesema kuwa gari hilo liliishiwa upepo, hivyo aliamua kuliingiza kwenye gema, ili kuepuka madhara zaidi.
