
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, amewavalisha nishani ya miaka 60 ya uhuru, nishani ya utumishi uliotukuka na nishani ya utumishi mrefu na tabia njema maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali 123 waliotunukiwa nishani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe Samia Suluhu Hassan.
