Back to top

Mbaroni kwa kukutwa na nyama ya twiga.

11 November 2019
Share

Jeshi  la  polisi  mkoani  Arusha limekamata jumla  ya watuhumiwa 9 wakiwemo vijana wawili  wakiwa wanatumia  jina la Gavana wa benki kuu ya Tanzania Prof Florence Luoga kufanya utapeli wa kuwaibia watu kwa njia  ya Mtandao.

Kamanda wa polisi wa  mkoa  wa Arusha Jonathan Shana amesema katika operesheni hiyo iliyofanywa kwa ushirikiano wa askari wa wanyamapori  kutoka TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro pia wamekamata Bunduki mbili za kivita risasi 15,majangili  wawili wakiwa na nyama ya twiga na wengine watano wakiwa na meno mawili ya Tembo.

Vitu vingine vilivyokamatwa ni pamoja na mashine ya kusajili line za Simu iliyokuwa inatumiwa  na vijana hao Juma Husein na Aman  Gabriel wanadaiwa pia kutumia hati ya kusafiria ya raia mmoja wa Australia kufanya utapeli huo.