Back to top

MCHENGERWA AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI PANGANI

21 January 2024
Share

Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, iliyopo mkoani Tanga, Bw.Isaya Mugishangwe Mbenje, kuanzia leo Januari 21, 2024, ili kupisha uchunguzi.
.
Hatua hiyo imefuata baada ya Mhe.Mchengerwa kupokea taarifa za Mkurugenzi huyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kusababisha kulega lega kwa utekelezaji wa miradi ya Maendeleo kwenye Halmashauri hiyo.