Back to top

Membe afukuzwa CCM, Kinana aonywa, Makamba asamehewa.

28 February 2020
Share

Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imemvua uanachama kada wake Bernad Membe huku ikitoa karipio kwa katibu mkuu mstaafu Abdulrahman Kinana na ikimsamehe katibu mkuu mwingine mstaafu Yusufu Makamba.

Katibu wa itikadi na uenezi wa halmashauri kuu ya chama hicho Humprey Polepole amesema uamuzi huo wa kamati kuu umefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa katiba ya chama hicho kulingana na makosa ambayo makada hao watatu walituhumiwa kuyafanya.
Kinana apewa karipio, awekwa chini ya uangalizi miezi 18.