Back to top

Mganga anayedaiwa kukinga majambazi wasikamatwe anaswa.

13 January 2020
Share

Jeshi la polisi mkoa wa Mara linawashikilia watu watano  kwa  tuhuma  za ujambazi akiwamo mganga wa kienyeji  ambaye anadaiwa kuwalinda watuhumiwa  hao  kwa kuwapa dawa za kienyeji  ili wasikamatwe wala kujulikana pale wanapofanya uhalifu.

 Akizungumza na waandishi wa habari Kamanada wa jeshi la polisi mkoa wa Mara ASP Daniel Shillah amesema watuhumiwa hao wamekamatwa wilaya ya Butiama wakiwa na mganga wao.